Ticker

6/recent/ticker-posts

YANGA SC YATOA DOZI NZITO, SINGIDA BIG STAR WAKILALA 4-1


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Yanga Sc wamerejea kileleni kwa kuiadhibu Singida Big Star kwa mabao 4-1 kwenye ligi kuu Tanzania Bara, mchezo ambao ulipigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini dar es Salaam,

Stori kubwa kwenye mchezo huo ni Fiston Kalala Mayele ambaye amefunga mabao matatu, Hat trick baada ya kukaa muda mrefu bila kufakamia nyavu kwenye ligi kuu inayoendelea huku goli lingine likifungwa na Kibwana Shomari.

Singida Big Star bao lao pekee lilifungwa na Meddie Kagere ambaye nae amekaa muda mrefu bila kufunga huku kwenye ligi kifikisha mabao mawili tu na kwa upande wa Fisto Mayele akifikisha mabao sita ndani ya ligi msimu huu.

Post a Comment

0 Comments