Ticker

6/recent/ticker-posts

AFYA NA USTAWI WA VIJANA NI CHACHU YA MAFANIKIO YA ELIMU

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kupitia mradi wake wa Haki Zetu, Maisha yetu, Mustakabali Wetu unaofahamika kama O3 Plus, likishirikiana na Chuo kishiriki cha elimu Dar es Salaam (DUCE) limekabidhi jengo la kituo cha ushauri nasihi na jengo maalum kwa ajili ya vijana katika kituo cha afya chuoni hapo ili kuboresha utoaji wa huduma rafiki kwa vijana.

Uboreshaji wa jengo maalum la vijana katika kituo cha afya na jengo la utoaji ushauri nasihi (council unit) umefadhiliwa na UNESCO kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma za afya na ushauri nasihi zinazokidhi mahitaji ya vijana.

“UNESCO inaamini kwamba maboresho haya yataongeza hamasa kwa vijana katika kupata taarifa na huduma za afya hivyo kuwawezesha kutunza na kujali afya zao.Hii itasaidia vijana kuwa na afya bora na kuweza kushiriki kikamilifu katika shughuli zao za kielimu na zile za maendeleo kwa ujumla ” anasema Bw. Mathias Luhanya-Mkuu wa Programu ya Afya na Ustawi kutoka UNESCO

Maboresho haya katika utoaji wa huduma za afya yanafanyika pia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (kampasi ya Mwalimu Nyerere) na Chuo Kikuu cha Dodoma na ni ishara kuwa Mradi umelenga katika kuacha alama ya kudumu inayogusa maisha ya vijana moja kwa moja.

Aidha, mbali na uboreshaji wa huduma hizi za afya, kupitia Mradi huu wa O3 Plus, zaidi ya wanafunzi 100,000 waliopo katika vyuo vikuu 17 hapa nchini wanategemewa kunufaika na afua mbalimbali zikiwemo zile za uanzishwaji wa madawati ya jinsia vyuoni, utoaji wa elimu ya kina ya stadi za maisha zinazozingatia VVU/UKIMWI, Afya ya uzazi na jinsia na matumii sahihi ya rasilimali (CSE) kupitia kozi mtandao na waelimisha rika, pamoja na utoaji wa mafunzo kwa watoa huduma za afya juu ya utoaji wa huduma rafiki za afya kwa vijana.
Mkuu wa Ofisi UNESCO, Bw.Michael Toto akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Jengo la Kituo cha Afya katika Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), uzinduzi ambao umefanyika Mei 25,2023 Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Ofisi UNESCO, Bw.Michael Toto (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Wawakilishi kutoka Wizara ya Elimu katika Mkutano wa Tatu wa Mwaka wa Kitaifa wa Kamati Tendaji ya Mradi wa O3 Plus uliofanyika Mei 25,2023 DUCE Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Ofisi UNESCO, Bw.Michael Toto (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Washiriki wa Mkutano wa Tatu wa Mwaka wa Kitaifa wa Kamati Tendaji ya Mradi wa O3 Plus uliofanyika Mei 25,2023 DUCE Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Ofisi UNESCO, Bw.Michael Toto (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Waratibu wa Mradi wa O3 Puls katika Mkutano wa Tatu wa Mwaka wa Kitaifa wa Kamati Tendaji ya Mradi wa O3 Plus uliofanyika Mei 25,2023 DUCE Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Ofisi UNESCO, Bw.Michael Toto akizungumza katika Mkutano wa Tatu wa Mwaka wa Kitaifa wa Kamati Tendaji ya Mradi wa O3 Plus uliofanyika Mei 25,2023 DUCE Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Programu ya Afya na Ustawi kutoka UNESCO Bw.Mathias Luhanya akizungumza katikaMkutano wa Tatu wa Mwaka wa Kitaifa wa Kamati Tendaji ya Mradi wa O3 Plus uliofanyika Mei 25,2023 DUCE Jijini Dar es Salaam
Msimamizi wa Mradi wa O3 Plus Dar es Salaam, Dkt.Alfred Msasu akiwasilisha Mada yake katika Mkutano wa Tatu wa Mwaka wa Kitaifa wa Kamati Tendaji ya Mradi wa O3 Plus uliofanyika Mei 25,2023 DUCE Jijini Dar es Salaam
Msimamizi wa Mradi Mkoa wa Dodoma Bw.Faraja Msangi akiwasilisha Mada yake katika Mkutano wa Tatu wa Mwaka wa Kitaifa wa Kamati Tendaji ya Mradi wa O3 Plus uliofanyika Mei 25,2023 DUCE Jijini Dar es Salaam
Bw.Clement Kihinga kutoka HISP akiwasilisha Mada yake katika
Mkutano wa Tatu wa Mwaka wa Kitaifa wa Kamati Tendaji ya Mradi wa O3 Plus uliofanyika Mei 25,2023 DUCE Jijini Dar es Salaam

Post a Comment

0 Comments