Ticker

6/recent/ticker-posts

WAZALISHAJI WA CHUMVI MTWARA WATAKIWA KUZALISHA CHUMVI KWA KUZINGATIA VIWANGO

WAZALISHAJI wa Chumvi mkoani Mtwara wametakiwa kuendelea kuzalisha na kufungasha chumvi iliyo bora kwa kuzingatia viwango, ubora na usalama ili kulinda afya ya mlaji pamoja na kupata masoko mengi ndani na nje ya nchi.

Wito huo umetolewa leo Novemba 1,2023 na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas wakati akifungua mafunzo kwa wadau wa chumvi kutoka katika Mkoa wa Mtwara.

Amesema mafunzo hayo yametokana na maombi ya wadau hao kupitia vikao mbalimbali vya kamati jumuishi ya kutatua changamoto za sekta ya chumvi nchini. Vikao hivyo vilijumuisha taasisi mbalimbali ikiwa ni pamoja na TBS.

"Mafunzo haya yamekuja kwa wakati muafaka ambapo Serikali imeazimia kwa dhati kuendeleza viwanda ili kutoa ajira katika kada mbalimbali pamoja na kuziwezesha bidhaa zetu kushindana katika masoko ya ndani, kikanda na ya kimataifa ". Amesema

Aidha ameipongeza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa maandalizi mazuri ya mafunzo na ameomba utaratibu wa kufanya mafunzo kama hayo kwa wadau wa chumvi uwe endelevu.

Pamoja na hayo amesema kuwa azma ya serikali ni kukuza sekta ya viwanda ili tuweze kujitosheleza katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.

Kwa upande wake Meneja wa kanda ya kusini (TBS), Mhandisi Saidi Mkwawa amesema lengo la mafunzo haya ni kuhakikisha wadau wa chumvi wanakuwa na uelewa na kuzalisha chumvi iliyokidhi ubora.

‘Katika mafunzo haya tumewashirikisha pia wadau muhimu ambao ni TIRDO na SIDO ili kuhakikisha elimu hii inakuwa na tija zaidi na mwisho wa siku muweze kuzalisha bidhaa bora’ alisema Mkwawa.

Mafunzo haya yatafanyika pia mkoani Lindi siku ya kesho Novemba 2,2023
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas akizungumza wakati akifungua Mafunzo  kwa wadau wa chumvi kutoka katika Mkoa wa Mtwara leo Novemba 1,2023.
Meneja wa TBS kanda ya kusini Mhandisi Said Mkwawa akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa wadau wa chumvi kutoka katika Mkoa wa Mtwara leo Novemba 1,2023.

Post a Comment

0 Comments