Ticker

6/recent/ticker-posts

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ELIMU YARIDHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA COSTECH

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo imeridhishwa na utendaji kazi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na matumaini yao kuona fedha wanazopatiwa zinafanya kazi iliyokusudiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 20,2024 Jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Mussa Sima amesema kuwa wametembelea tume hiyo na kujiridhisha kwa juhudi wanazozifanya hasa kwenye masuala ya utafiti ambazo zimekuwa zikiibuliwa na wataalamu nchini.

"Tumeona kazi nzuri sana inafanyika kwa ajili ya utafiti na utafiti huu si wa Elimu tu unagusa maeneo yote, tumeona hata kwenye kilimo wameshirikiana na Taasisi ya chuo Kikuu Cha Kilimo Sokoine (SUA) kwenye maabara yao wameandaa vipimo vya kupima afya ya udongo". Amesema Mhe. Sima

Aidha amesema kuwa katika sekta ya Elimu kuna mabadiliko makubwa kupitia mtaala mpya ambao utaleta mapinduzi makubwa wakati ambao serikali inaandaa sera na sheria ambazo zitasaidia kuondokana na changamoto za kukosa walimu wa masomo ya sayansi,uhandisi na hisabati ili kuongeza umahiri kwa wanafunzi waweze kujiajiri na kuajiriwa.

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu amesema kuwa wataendelea kufanya jitihada zao kufadhili kupitia pesa wanazopatiwa ili kufanya Tafiti ambazo zitarudisha matokeo chanya kwa jamii ambapo pia watatumia matokeo wanayo yapata kuisaidiaa serikali.

Aidha Dkt. Nungu ameeleza kuwa wanafanya tafiti ya matumizi ya Teknolojia ya Akili bandia ambapo wanatarajia kupata matokeo baada ya miaka miwili kwa ajili ya matumizi halisia ya kila siku.

"Tunategemea baada ya miaka miwili kupata matokeo ya akili bandia (Artificial intelligence) sio tu kwa masuala ya mtandaoni lakini kwa maisha halisia, kama nchi tunafadhili tafiti katika maeneo hayo". Ameeleza.

Pamoja na hayo Dkt. Nungu amewaalika vijana kuleta kazi zao bunifu kuzionesha ili waweze kuinuka kiuchumi na kukidhi mahitaji yao kwa lengo la kuongeza ajira na kuokoa kupeleka nje fedha za kigeni.
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo ilipotembelea ofisi za (COSTECH) leo 20, 2024 Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu akimpokea Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe. Mussa Sima mara baada ya kamati hiyo kuwasili katika ofisi za (COSTECH) leo 20, 2024 Jijini Dar es Salaam
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe. Mussa Sima akizungumza kwenye kikao cha kamati hiyo na Menejimenti ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) mara baada ya kamati hiyo kutembelea ofisi za (COSTECH) leo 20, 2024 Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo pamoja na Menejimenti ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) mara baada ya kamati hiyo kutembelea ofisi za (COSTECH) leo 20, 2024 Jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anayehusika na Elimu, Dkt. Franklin Jasson Rwezimula akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo pamoja na Menejimenti ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) mara baada ya kamati hiyo kutembelea ofisi za (COSTECH) leo 20, 2024 Jijini Dar es Salaam
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo wakichangia jambo kwenye kikao na Menejimenti ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) mara baada ya kamati hiyo kutembelea ofisi za (COSTECH) leo 20, 2024 Jijini Dar es Salaam
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe. Mussa Sima akiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anayehusika na Elimu, Dkt. Franklin Jasson Rwezimula pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo mara baada ya kutembelea ofisi za (COSTECH) leo 20, 2024 Jijini Dar es Salaam
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe. Mussa Sima akiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anayehusika na Elimu, Dkt. Franklin Jasson Rwezimula pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu wakiwa kwenye picha ya pamoja na Menejimenti ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) mara baada ya kamati hiyo kutembelea ofisi za (COSTECH) leo 20, 2024 Jijini Dar es Salaam.


(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

Post a Comment

0 Comments